KLERUU

KLERUU
KLERUU

Ibada

Ibada

Tuesday, April 26, 2016

Lucy Kibaki afariki

Lucy kibaki na mkewe wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2007

Lucy Kibaki na mumewe Mwai KIbaki wakiwapungia mkono wafuasi wao mda mchache baada ya kibaki kuwasilisha stakhabadhi zake za uchaguzi katika tume ya uchaguzi mwaka 2007.Picha ni kwa niaba ya Getty images

Lucy Kibaki na mumewe aliyekuwa rais wa Kenya Mwai Kibaki pamoja na mkewe marehemu Kijana Wamalwa wakati wa misa ya kifo cha Wamalwa.Picha kwa niaba ya Getty Images

Aliyekuwa mke wa rais wa zamani nchini Kenya Lucy Kibaki amefariki.

Lucy alifariki katika hospitali ya Bupa Cromwell mjini London. Alisafrishwa hadi mjini Landon wiki moja iliopita kwa matibabu.

Akithibitisha kifo chake rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema kuwa kenya imesikitishwa na kifo cha mama Lucy mke wa aliyekuwa rais wa Kenya Mwai Kibaki.

Katika taarifa iliotumwa katika vyombo vya habari Uhuru amesema bi Lucy amekuwa mgonjwa kwa kipindi cha mwezi mmoja.

Amesema kuwa Kenya imempoteza mwanamke aliyechangia mengi katika maendeleo ya taifa la Kenya hususan katika vita dhidi ya ugonjwa wa ukimwi.

Rais ametuma risala za rambi rambi kwa mtangulizi wake Mwai Kibaki pamoja na familia yake.

Chanzo: bbc swahili

Saturday, April 16, 2016

Wakenya waliofikishwa ICC wafurahia uhuru

Wakenya hao wamesisitiza kwamba hawakuhusika katika ghasia hizo
Wakenya sita waliokuwa wamefunguliwa mashtaka na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC) kuhusiana na ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa 2007 wamekusanyika kwa mkutano wa maombi mjini Nakuru kusherehekea kutamatishwa kwa kesi dhidi ya Naibu Rais William Ruto na mwanahabari Joshua Sang.

Mji wa Nakuru unapatikana katika uliokuwa mkoa wa Bonde la Ufa na uliathirika sana wakati wa mapigano hayo.

Rais Uhuru Kenyatta, aliyekuwa miongoni mwa waliofunguliwa mashtaka, amekuwa akihimiza maridhiano na umoja.

Wengine waliokuwa wamefunguliwa mashtaka ni aliyekuwa mkuu wa polisi Meja Jenerali Hussein Ali, aliyekuwa mkuu wa utumishi wa umma Francis Muthaura na waziri wa zamani Henry Kosgey.

Watu takriban 1,300 walifariki na wengine 600,000 wakafurushwa makwao, wengi wao eneo la Bonde la Ufa, wakati wa mapigano hayo.

Wakenya sita walikuwa wamefunguliwa mashtaka ICC
Mahakama ya ICC awali ilithibitisha mashtaka dhidi ya Bw Kenyatta, Bw Ruto na Bw Sang lakini kesi dhidi ya Bw Kenyatta ikaondolewa Desemba mwaka 2014.

Kesi dhidi ya Bw Ruto na Bw Sang ilitamatishwa na majaji mapema mwezi huu.

Mwendesha mashtaka mkuu wa mahakama ya ICC Fatou Bensouda alikuwa amelalamika kwamba mashahidi wengi wamehongwa au kutishwa na wakabadilisha ushahidi waliokuwa wametoa awali na wengine wakajiondoa.
Wakati wa kutamatisha kesi dhidi ya Bw Ruto na Bw Sang tarehe 5 Aprili, Jaji Chile Eboe-Osuji kwenye uamuzi wake alisema huenda kuingiliwa kwa mashahidi kulidhoofisha kesi hiyo.

Aidha, alisema kulikuwa na uingiliaji wa kisiasa ambao huenda uliwatia hofu baadhi ya mashahidi.

Monday, April 11, 2016

Watumishi hewa wamponza mkuu wa Mkoa

Rais Magufuli aliwaagiza wakuu wa mikoa wafanye uchunguzi kuwatambua watumishi hewa
Rais wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa mkuu wa mkoa wa Shinyanga kutokana na kuwepo kwa watumishi hewa.

Anna Kilango Malecela alitangaza kwenye vyombo vya habari kuwa mkoa wake hakuwa na watumishi hewa.

Ikulu hata hivyo ilifanya uchunguzi wake na kubaini kuwepo kwa wafanyakazi hewa 45 katika awamu ya kwanza.

Awamu ya pili ya uchunguzi huo bado inaendelea katika wilaya mbili za Ushetu na Shinyanga Vijijini ambapo jumla ya wafanyakazi 2,000 wamegunduliwa nchini Tanzania kwa awamu ya kwanza jambo ambalo Rais Magufuli anataka limalizwe mara moja.

Akiongea Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli amesema amesikitishwa na hali hiyo na kuagiza mkuu huyo wa mkoa na Katibu Tawala wa Mkoa Abdul Rashid Dachi kuondolewa kazini mara moja.

"Na wale wote wa Shinyanga ambao walisemekana ni zero, hakuna mtumishi hewa, walikuwa tayari wameshalipwa shilingi milioni 339.9, nimejiuliza sana, na nikajiuliza sana na kwa kweli nimejiuliza sana na kwa masikitiko makubwa, kwa nini mkuu wa mkoa alisema hakuna mtumishi hewa?" amesema Dkt Magufuli.

Kwa jumla, zaidi ya wafanyakazi hewa 2,000 waligunduliwa baada ya utathmini kufanywa mikoani.


Chanzo: bbc swahili

Friday, April 8, 2016

Uliwahi kuona Teja akiibiwa na kibaka?

Mwenye jaketi la njano ni kibaka na waliomkwida ni mateja wakimvuta kumpeleka polisi. Hapa ni mkabala na jengo la NSSF Manispaa ya Iringa


 KUNA usemi usemwao “mwizi akiibiwa, polisi hawalali”. Usemi huu si wakudhania wala wakufikirika.

Ilikuwa majira ya saa 6:27 mchana nilipowaona watu wakivutana mashati katikati ya barabara mkabala na jingo la Tanesco Manispaa ya Iringa hali ambayo kwa haraka sikuelewa.

Niliamua kusogea karibu kuuliza kinachoendelea nikaambiwa kibaka kamuibia teja ikabidi mateda wamkamate ili waanze kumshughulikia.

Mateja hao walimvuta kibaka huyo ng’ambo ya barabara wakampa kichapo kasha wakamkuda kuelekea naye kituo cha Polisi.

Wakati wakielekea kituo cha polisi kibaka akawa anaomba msamaha lakini mateja hao hawakutaka kumsikiliza zaidi ya kumchapa na kumsukuma kuelekea kituo cha polisi.

Haikuwa kazi rahisi kwa kibaka huyo kujieleza kwa kwa kuwa mateja hawakuta kusikia maelezo bali walitaka afikishwe mahakamani na kasha walihakakisha wanafka kituo cha polisi na kutiwa mikononi mwa polisi ili kazi ibaki kwa polisi

Wednesday, March 30, 2016

Waziri Mahiga akosolewa kutowaweka wazi watanzania juu ya fedha za MCC





Waziri Kivuli wa Mambo ya Nje Mch. Peter Msigwa akiongea na waandishi wa habari juu ya fedha za MCC.



SIKU chache baada ya Serikali ya Marekani kuzuia fedha za msaada kwa ajili ya maendeleo Millennium Challenge Cooperation (MCC), msemaji kambi rasmi ya upinzani Waziri kivuli wa Wizara wa Mambo ya Nje Mch. Peter Msigwa ametoa tamko la kuwataka Jumuiya ya Ulaya nayo kuzuia misaada kwa serikali Tanzania iweze kujitafakari kama imezingatia vigezo vya MCC katika kupata misaada.

Akizungumza na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa Hotel ya M. R, Mch. Msigwa ambaye pia ni Mbubge wa Jimbo la Iringa Mjini alisema kambi ya upinzani imesikitishwa na maelezo ya Waziri wa Mambo ya Nje Balozi Agustino Mahiga kutowaeleza wazi watanzania sababu hasa ya serikli ya Marekani kusitisha utolewaji wa fedha hizo za msaada badala yake kukurupuka na kutoa sababu ambazo hazina mashiko kwa wananchi.

Amesema kuwa sababu ambazo Balozi Mahiga alizitoa juzi hazina mashiko kwa kuwa serikali ya Tanzania imekiuka misingi mojawapo inayozingatiwa na MCC katika vigezo 17 katika kuchagua nchi inayostahili kupata msaada na miongoni mwa vigezo vya msingi kabisa ni nchi husika kuwa na dhamira ya dhati ya kuimarisha demokrasia na kuendesha chaguzi zilizo huru na haki.

Amesema kuwa katika taarifa yake MCC ilieleza maeneo ambayo Tanzania imekiuka vigezo kuwa ni marudio ya uchaguzi haramu wa urais Zanzibar na kupitisha Sheria ya Makosa ya Mawasiliano ya Mitandaoni (Cyber Crime) sheria inayonyima uhuru wa wa kujieleza na uhuru wa kujumuika.

"Serikali ya Tanzania haijachukua hatua za kuhakikisha kuheshimiwa kwa uhuru wa kujieleza na uhuru wa kujumuika katika utekelezwaji wa sheria ya Uhalifu wa Mtandao , Tanzania iliendelea na uchaguzi wa marudio Zanzibar ambao haukushirikisha wote na wala haukuakisi maoni ya wote, licha ya malalamiko kutoka kwa serikali ya Marekani na jamii ya kimataifa”, amesema

Mchungaji Msigwa amesema kuwa kwa mantiki hiyo ni dhahiri kuwa Tanzania haikupaswa kushitushwa na uamuzi wa MCC kwa kuwa Serikali ilivifahamu vizuri na mapema vigezo vya kustahili kupewa misaada na MCC.

Aliongeza kuwa inashangaza na kusikitisha kuona Msomi na Mwanadiplomasia mzoefu kama Balozi Mahiga akilitia Taifa Aibu ya Mwaka kwa kulalamikia kuonewa na kutoa kauli za “hovyo” kama alivyozitoa.

Saturday, March 26, 2016

Binadamu amejipaka uchafu: Askofu Ngalalekumtwa




BINADAMU anaelezwa kuwa ni kiumbe kilichochafuka na uchafu wa kutisha ambao anahitaji msaada kwa ajili ya kusafishwa.

Haya yamezungumzwa na Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania Mhashamu askofu Tarcisius Ngalalekumtwa alipokuwa akihubiri katika Mkesha wa Pasaka Parokia ya Bikira Maria Consolata - Mshindo Jimbo la Iringa.

Askofu Ngalalekumtwa ambaye pia ni askofu wa jimbo la Iringa alisema binadamu amejaa maovu ya kila aina ambayo yamekuwa kikwazo kwa wengine na kusema kuwa bila nguvu ya Mungu mwanadamu pekee hayawezi.

Thursday, March 10, 2016

Baada ya mgogoro wa uchaguzi Uganda, waandishi wa habari wanahofia usalama wao wa kihabari




Yoweri Kaguta Museven
Mpiga picha wa muda mrefu nchini Uganda Abubaker Lubowa ametoa hisia zake jinshi ilivyomgharimu baada ya kupewa kazi na mhariri wake kuripoti habari za mpinzani wakati wa kampeni katika uchaguzi Mkuu Uganda akimripoti kiongozi wa upinzani Kizza Besigye.

Mwezi Februari 27,  Mwaka hu, Lubowa na mwenzake katika gazeti binafsi la Daily Monitor walikamatwa wakiwa katika harakati za kuandika habari za  kiongozi wa upinzani Besigye mji mkuu wa Uganda, ambapo Besigye amefungiwa tangu matokeo ya uchaguzi yalipotangazwa Februari 20.