KLERUU

KLERUU
KLERUU

Ibada

Ibada

Friday, May 20, 2016

Walioua watu msikitini Mwanza wasakwa

Shambulio lilitekelezwa wakati wa swala jioni
Polisi nchini Tanzania wanawazuilia watu watatu wanaotuhumiwa kuhusika shambulio katika msikiti mmoja mjini Mwanza magharibi mwa nchi hiyo.

Watu watatu, akiwemo Imam, walifariki wakati wa shambulio hilo lililotekelezwa katika msikiti wa Rahman wakati wa swala ya usiku siku ya Jumatano.

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi jijini humo, Ahmed Msangi, uchunguzi wa mwanzo umebaini kwamba mauaji hayo yalifanywa kwa kutumia mapanga na kuongeza kuwa, polisi wanachunguza chanzo cha shambulizi hilo.

Baadhi ya walioshuhudia tukio hilo, wamesema shambulio hilo lilitekelezwa na kundi la watu wasiopungua 15.
Hakuna aliyedai kuhusika katika shambulio hilo.

Tukio jingine la mauaji ya kutumia silaha pia limetokea katika mkoa wa Pwani wilaya ya Mkuranga ambapo askari polisi aliyefahamika kwa jina la Sajenti Kinyogoli ameuawa na watu wasiojulikana.

Matukio hayo yote yametokea wiki hii kulipoibuka taarifa kwenye mtandao wa Twitter juu ya kikundi kilichojitambulisha kama wafuasi wa mtandao wa kigaidi wa Islamic State wakifanya mazoezi eneo la Tanga, kaskazini mashariki mwa Tanzania.


Chanzo: bbc swahili

Monday, May 16, 2016

Kagame: Hatuwezi kumkamata Bashir

Rais wa Rwanda Paul Kagame ametangaza kwamba hakuna sababu hata moja itakayoifanya nchi yake kumkamata rais wa Sudan Omar al-Bashir ikiwa ataalikwa kuhudhuria kikao cha Umoja wa Afrika kitakachofanyika nchini Rwanda mwezi Julai mwaka huu.

Rais Bashir anasakwa na mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita (ICC) kwa tuhuma za uhalifu wa kivita na mauaji katika jimbo la Darfur.

Rwanda si mwanachama wa mahakama ya ICC.

Kutoka Kigali Yves Bucyana anaarifu.

Tuesday, May 10, 2016

Huduma ya mabasi ya mwendo wa kasi yaanza Dar


Abiria wakiwa wamepanda basi la BRT
Huduma ya mabasi ya uchukuzi yanayoenda kwa kasi BRT nchini Tanzania imeanza rasmi siku ya jumanne katika jiji la kibiashara la Dar es Salaam.

Abiria watalipa shilingi 400 na 800 huku wanafunzi wakilipa 200 kulingana na mamlaka ya uchukuzi wa barabarani na majini SUMATRA.

Mkurugenzi mkuu anayesimamia mamlaka hiyo bw Giliard Ngewe amewaambia maripota mjini humo kwamba nauli zitakuwa shilingi 400 kwa uchukuzi wa barabara ndogo,650 kwa barabara kuu na shilingi 800 kwa uchukuzi wa barabara kuu na ndogo huku wanafunzi wakilipa shilingi 200 kwa kila safari.

ASiku ya Jummanne na Jumatano mabasi hayo yatahudumu kati ya saa kumi na moja alfajiri na saa sita mchana.

Tunawaonya wanaoendesha pikipiki na madereva wa magari mengine kutotumia barabara za mradi wa BRT,alisema akiongezea kwamba bado wanazungumza na washikadau kutafuta njia nzuri ya kupanga barabara zitakazotumiwa na BRT na mabasi mengine ya abiria.

Kulingana na yeye,mfumo huo wa BRT hauyaruhusu mabasi mengine kutoa huduma pamoja na mabasi ya BRT kwa hivyo abiria walioko katika barabara za BRT hawataruhusiwa kutumia mabasi mengine.

Chanzo: bbc swahili 

Tuesday, April 26, 2016

Lucy Kibaki afariki

Lucy kibaki na mkewe wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2007

Lucy Kibaki na mumewe Mwai KIbaki wakiwapungia mkono wafuasi wao mda mchache baada ya kibaki kuwasilisha stakhabadhi zake za uchaguzi katika tume ya uchaguzi mwaka 2007.Picha ni kwa niaba ya Getty images

Lucy Kibaki na mumewe aliyekuwa rais wa Kenya Mwai Kibaki pamoja na mkewe marehemu Kijana Wamalwa wakati wa misa ya kifo cha Wamalwa.Picha kwa niaba ya Getty Images

Aliyekuwa mke wa rais wa zamani nchini Kenya Lucy Kibaki amefariki.

Lucy alifariki katika hospitali ya Bupa Cromwell mjini London. Alisafrishwa hadi mjini Landon wiki moja iliopita kwa matibabu.

Akithibitisha kifo chake rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema kuwa kenya imesikitishwa na kifo cha mama Lucy mke wa aliyekuwa rais wa Kenya Mwai Kibaki.

Katika taarifa iliotumwa katika vyombo vya habari Uhuru amesema bi Lucy amekuwa mgonjwa kwa kipindi cha mwezi mmoja.

Amesema kuwa Kenya imempoteza mwanamke aliyechangia mengi katika maendeleo ya taifa la Kenya hususan katika vita dhidi ya ugonjwa wa ukimwi.

Rais ametuma risala za rambi rambi kwa mtangulizi wake Mwai Kibaki pamoja na familia yake.

Chanzo: bbc swahili

Saturday, April 16, 2016

Wakenya waliofikishwa ICC wafurahia uhuru

Wakenya hao wamesisitiza kwamba hawakuhusika katika ghasia hizo
Wakenya sita waliokuwa wamefunguliwa mashtaka na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC) kuhusiana na ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa 2007 wamekusanyika kwa mkutano wa maombi mjini Nakuru kusherehekea kutamatishwa kwa kesi dhidi ya Naibu Rais William Ruto na mwanahabari Joshua Sang.

Mji wa Nakuru unapatikana katika uliokuwa mkoa wa Bonde la Ufa na uliathirika sana wakati wa mapigano hayo.

Rais Uhuru Kenyatta, aliyekuwa miongoni mwa waliofunguliwa mashtaka, amekuwa akihimiza maridhiano na umoja.

Wengine waliokuwa wamefunguliwa mashtaka ni aliyekuwa mkuu wa polisi Meja Jenerali Hussein Ali, aliyekuwa mkuu wa utumishi wa umma Francis Muthaura na waziri wa zamani Henry Kosgey.

Watu takriban 1,300 walifariki na wengine 600,000 wakafurushwa makwao, wengi wao eneo la Bonde la Ufa, wakati wa mapigano hayo.

Wakenya sita walikuwa wamefunguliwa mashtaka ICC
Mahakama ya ICC awali ilithibitisha mashtaka dhidi ya Bw Kenyatta, Bw Ruto na Bw Sang lakini kesi dhidi ya Bw Kenyatta ikaondolewa Desemba mwaka 2014.

Kesi dhidi ya Bw Ruto na Bw Sang ilitamatishwa na majaji mapema mwezi huu.

Mwendesha mashtaka mkuu wa mahakama ya ICC Fatou Bensouda alikuwa amelalamika kwamba mashahidi wengi wamehongwa au kutishwa na wakabadilisha ushahidi waliokuwa wametoa awali na wengine wakajiondoa.
Wakati wa kutamatisha kesi dhidi ya Bw Ruto na Bw Sang tarehe 5 Aprili, Jaji Chile Eboe-Osuji kwenye uamuzi wake alisema huenda kuingiliwa kwa mashahidi kulidhoofisha kesi hiyo.

Aidha, alisema kulikuwa na uingiliaji wa kisiasa ambao huenda uliwatia hofu baadhi ya mashahidi.

Monday, April 11, 2016

Watumishi hewa wamponza mkuu wa Mkoa

Rais Magufuli aliwaagiza wakuu wa mikoa wafanye uchunguzi kuwatambua watumishi hewa
Rais wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa mkuu wa mkoa wa Shinyanga kutokana na kuwepo kwa watumishi hewa.

Anna Kilango Malecela alitangaza kwenye vyombo vya habari kuwa mkoa wake hakuwa na watumishi hewa.

Ikulu hata hivyo ilifanya uchunguzi wake na kubaini kuwepo kwa wafanyakazi hewa 45 katika awamu ya kwanza.

Awamu ya pili ya uchunguzi huo bado inaendelea katika wilaya mbili za Ushetu na Shinyanga Vijijini ambapo jumla ya wafanyakazi 2,000 wamegunduliwa nchini Tanzania kwa awamu ya kwanza jambo ambalo Rais Magufuli anataka limalizwe mara moja.

Akiongea Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli amesema amesikitishwa na hali hiyo na kuagiza mkuu huyo wa mkoa na Katibu Tawala wa Mkoa Abdul Rashid Dachi kuondolewa kazini mara moja.

"Na wale wote wa Shinyanga ambao walisemekana ni zero, hakuna mtumishi hewa, walikuwa tayari wameshalipwa shilingi milioni 339.9, nimejiuliza sana, na nikajiuliza sana na kwa kweli nimejiuliza sana na kwa masikitiko makubwa, kwa nini mkuu wa mkoa alisema hakuna mtumishi hewa?" amesema Dkt Magufuli.

Kwa jumla, zaidi ya wafanyakazi hewa 2,000 waligunduliwa baada ya utathmini kufanywa mikoani.


Chanzo: bbc swahili

Friday, April 8, 2016

Uliwahi kuona Teja akiibiwa na kibaka?

Mwenye jaketi la njano ni kibaka na waliomkwida ni mateja wakimvuta kumpeleka polisi. Hapa ni mkabala na jengo la NSSF Manispaa ya Iringa


 KUNA usemi usemwao “mwizi akiibiwa, polisi hawalali”. Usemi huu si wakudhania wala wakufikirika.

Ilikuwa majira ya saa 6:27 mchana nilipowaona watu wakivutana mashati katikati ya barabara mkabala na jingo la Tanesco Manispaa ya Iringa hali ambayo kwa haraka sikuelewa.

Niliamua kusogea karibu kuuliza kinachoendelea nikaambiwa kibaka kamuibia teja ikabidi mateda wamkamate ili waanze kumshughulikia.

Mateja hao walimvuta kibaka huyo ng’ambo ya barabara wakampa kichapo kasha wakamkuda kuelekea naye kituo cha Polisi.

Wakati wakielekea kituo cha polisi kibaka akawa anaomba msamaha lakini mateja hao hawakutaka kumsikiliza zaidi ya kumchapa na kumsukuma kuelekea kituo cha polisi.

Haikuwa kazi rahisi kwa kibaka huyo kujieleza kwa kwa kuwa mateja hawakuta kusikia maelezo bali walitaka afikishwe mahakamani na kasha walihakakisha wanafka kituo cha polisi na kutiwa mikononi mwa polisi ili kazi ibaki kwa polisi