KLERUU

KLERUU
KLERUU

Ibada

Ibada

Monday, November 30, 2015

Papa 'wakristu wasilipize kisasi' Afrika ya Kati

Papa Francis ambaye yuko nchini Jamhuri ya Afrika ya kati amezuru msikiti mmoja katika mji mkuu wa Bangui.

Msikiti huo wa Koudoukou uko katikati ya mji wa Bangui uliosakamwa na vita vya kidini kati ya wakristu na waislamu.

Papa Francis alikutana na waislamu waliokwama katika sehemu ya mji unaojulikana na PK5, eno ambao umezingiriwa na wapiganaji wa Kikristu waliojihami vikali wa Anti-Balaka.

Asili mia kubwa ya takriban waislamu laki moja nchini humo, walikimbia mji huo kufuatia mapigano yaliyodumu kwa ziaidi ya miaka mitati.

Misikiti mingi iliharibiwa wakati wa vita hivyo.

Papa Francis amewataka wasameheane na waache kulipiza kisasi.

''Wakristo na Waislamu ni ndugu ,hakuna faida yeyote inayotokana na uhasama''alisema papa.

''hatupaswi kulipiza kisasi na kumdhuru mtu yeyote kwa jina la mungu'' alisema Papa Francis.

Hivi sasa leo Papa Francis anaongoza misa yake ya mwisho barani Afrika katika uwanja mkuu wa kitaifa ambako anatarajiwa kutoa wito wa maridhiano, amani na utengamano.

Saturday, August 1, 2015

Mabaki ya MH370 yasafirishwa Ufaransa

Mabaki ya MH370 yasafirishwa Ufaransa
Mabaki kutoka kwa ndege ya Boeng 777 yanayoaminiwa kutoka kwa ndege iliyotoweka ya shirika la ndege la Malaysia ya MH370 yamesafiriswa kwenda nchini ufaransa kufanyiwa uchunguzi.

Sehemu ya mbawa la ndege hiyo ilianguka katika kisiwa cha Reunion katika habari ya Hindi ambapo ilipatikana siku ya Jumatano.

Mabaki hayo yatachunguzwa katika mahabara ya wizara ya ulinzi katika mji ulio kusini wa Toulause wiki ijayo.

Boeng inatuma kundi la wataalmu kusadia uchunguzi huo.

Ndege ya MH370 ilitoweka mwezi machi mwaka 2014 ikiwa na abiria 239.



Chanzo: bbc swahili

Saturday, July 25, 2015

Matokeo ya kura za maoni Chadema kwa baadhi ya majimbo






JIMBO la Kilolo kwa mara ya kwanza limefanya upigaji wa kura za maoni kupitisha mgombea wa ubunge kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambapo wajumbe wamejivunia kumpata mgombea shupavu anayejiamini na kwamba ana nguvu kubwa ya kushinda katika uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 Mwaka huu.

Katika uchaguzi huo jumla ya wapiga kura walikuwa 240 ambapo Brian Kikoti aliibuka kwa ushindi wa kura 215, Ahaz Challi 12, Samson Mnyawami  9, Edger Kihwelo 2, Hezlon Lusapi 2.

Mufindi Kusini: Frank Malata 69, Oliva Lema 27, Crepton Madunda 18 Mustafa Msovera 12 jumla ya kura 126.

Jimbo la Isimani: Patrick Ole Sosopi 101, Widmani Masika 31 jumla ya kura zote ni 142 wakati Iringa Mjini: Mch. Peter Msigwa 177, Leonce Marto 18 huku kura 1 ikiharibika na jumla ya kura zote 196.

Kwa upande wa Jimbo jipya la Mafinga; Jeofrey Mungai ameibuka mshindi.

Ludewa: Okol Haule 181, Batromeyo Mkinga 126, David Msanga 3. Njombe Kusini: Emmanuel Masonga 92, Emilian Msigwa 41, Fukh Lulandala 13, Ally Mhagama 3, Alatanga Nyagawa 1, Stanislaus Mdetele 2,  Emmanuel Filangali 1, Lucia Mlowe 0. Viti maalum Rose Mayemba.

Makete: Jackson Mbogela 143, Ahadi Mtweve 77, Meck Emmanuel  9, Hadson Mrema 8, Benjamini Bukuku 1, Abiud Mwandikilwa 0.

Akihutubia mara baada ya kutangazwa mshindi kuwa mgombea ubunge katika jimbo la Kilolo Brian Kikoti alisema kwa ushindi alioupata ameamini kuwa anahitajika na kwamba anayo kazi ya kufanya ili asiwaangushe wajumbe waliompigia kura na wananchi kwa ujumla.

“Mmenionesha kuwa mnanihitaji. Tunakwenda kushinda uchaguzi katika ngazi ya udiwani, ubunge hadi urais. Sitawaangusha ndugu zangu” alisema Kikoti.

Saturday, June 20, 2015

CCM ni jinamizi linalotakiwa kuondolewa: Mbunge

Mbunge wa viti maalum wa jimbo la Mjini Magharibi – Zanzibar Maryam Salum Msabaha aliyejitanda nguo kichwani akisikiliza kwa umakini namna watoto wanavyolelewa. Mwenye kofia ni Sista Cecilia kitasile mlezi wa watoto hao.




BARAZA la wanawake wa Chama cha Demkrasia na Maendeleo (Bawacha) Mkoa wa Iringa wametoa msaada wa vitu mbalimbali katika kituo cha watoto yati cha Mersino Meraddin Migoli pamoja na fedha tasilimu kiasi cha shilingi 1,645,000/=.

Msaada huo umetolewa wakati walipotembelea kituoni hapo kama ni sehemu ya kufanya kumbukumbu ya mtoto wa Afrika.

Wakikabidhi msaada huo, Mbunge wa viti maalum wa jimbo la Mjini Magharibi – Zanzibar Maryam Salum Msabaha alibubujikwa na machozi baada ya kuwaona watoto hao na kutoa msaada wa shilingi milioni moja huku Mbunge wa viti maalum Naomi Kaihula akitoa kiasi cha shlingi 550,000/=.

Akizungumza kituoni hapo Maryam Msabaha alisema jamii ina jukumu la kuishi na watoto wasio na wazazi kama familia ili kuwajenge uwezo wa kutengeneza maisha yao kimalezi.

Alisema suala la kulea watoto si la wamisionari pekee bali ni jukumu la kila mtu aliyeumbwa na Mwenyezi Mungu na kwamba watoto wasibaguliwe.

Wednesday, May 20, 2015

Polisi wadaiwa kuua raia mmoja huku wawili wakijeruhiwa

NA MWANDISHI WETU, NJOMBE.

RAIA mmoja mkazi wa Njombe mjini ameuawa kwa risasi na Polisi kitendo kilichowatia hasira wananchi na kufunga mitaa kwa maandamano mkoani Njombe kwa kutaka kujua sababu zilizowafanya Polisi kufyatua risasi kwa wananchi na kusababisha kifo cha mwanachi huyo.

Kutokana na tukio hilo wananchi waliamua kufanya maandamano leo kutaka kujua sababu za mwezao kuuawa jambo lililosababisha jeshi la polisi kutumia mabomu na silaha za moto hapo na kujeruhi raia wengine wawili katika maandamano hayo.

Hasira za wananchi hao zimesababisha shughuli kusimama kwa siku nzima huku maduka yakifungwa pamoja na usafiri kuwa mgumu kutokana na wananchi kutaka kupata majibu ya kuuawa kwa  raia huyo.

Wakizungumza na mtandao huu, wananchi wakazi wa Njombe wamesema Polisi walifika kilabuni walikokuwa wakinywa pombe wananchi na kufyatua risasi bila sababu yoyote kisha kumpiga mwananchi huyo aliyefariki dunia papo hapo.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo Amos Nziku ameeleza kuwa, ilikuwa majira ya jioni jana walipokuwa wakipata vinywaji katika kilabu kimoja cha pombe ambapo alitokea raia mmoja akaingia kilabuni hapo akikimbia jambo lililowashtusha na kumtaka kueleza sababu ya kuingia akiwa anakimbia.

“Jana tulikuwa kilabu cha Nyondo tukipata kiburudisho chetu cha koo huku tukiongea na marafiki gafla akaingia mtu akikimbia tukashtuaka sana. Sasa kule kushtuka kila mtu akataka kujua anakimbia nini, yule jamaa akatuambia polisi wanamfukuza.

“Tulitoka watu wote pale kilabuni kuangalia tukawaona kweli polisi tukaanza kuwapigia kelele kutaka kujua ni kwa nini wanamfukuza. Lengo ni kujua kama ni mwizi ili tumshughulikie lakini cha kushangaza, polisi wakaanza kufyatua risasi kuelekeza kwetu. Kwa bahati mbaya risasi ilimfikia mwenzetu mmoja akafariki papo hapo” amesema Nziku.

Monday, April 20, 2015

Zwelithini kutuliza raia Afrika Kusini

Goodwill Zwelithini, Mflame wa Zulu
Mfalme wa Jamii wa Wazulu nchini Afrika Kusini, Goodwill Zwelithini, anatarajiwa kutoa wito kwa raia wa nchi hiyo kujiepusha na ghasia, kufuatia kuongezeka kwa mashambulio ya kibaguzi nchini humo.

Mfalme huyo ameshutumiwa kwa kuchochea mashambulio hayo ambayo yamesababisha vifo vya watu saba.

Zwelithini, alinukuliwa akisema kuwa raia wote wa kigeni wanapaswa kurejea katika mataifa yao.

Zaidi ya watu mia tatu wamekamatwa kuhusiana ghasia hizo.

Maelfu ya watu wanatarajiwa kufurika uwanja mmoja ulioko mji wa Mashariki wa Durban kusikiliza hotuba hiyo ya Mfalme Zwelithini.

Amekariri kuwa matamshi yake hayakufahamika.

Miongoni mwa washukiwa waliokamatwa hivi karibuni na wanaume watatu ambao wanatuhumiwa kuhusika na mauaji ya rais mmoja wa Mozambique katika eneo la Alexandra viungani mwa mji mkuu wa Johannesburg.

Picha kadhaa zimeonyesha Emmanuel Sithole akindungwa kisu huku umati mkubwa ukitizama.

Raia moja wa kigeni akishambuliwa nchini Afrika Kusini
Mama mmoja raia wa kigeni ambaye nyumba yake ilivamiwa nchini Afrika Kusini

Rais wa nchi hiyo Jacob Zuma, amesema mashambulio hayo yanakwenda kinyume na maadili yote wanayoamini.

Makundi kadhaa yaliyojihami yameshambulia na kupora maduka kadhaa yanayomilikiwa na wahamiaji kutoka mataifa mengine ya Afrika.

Huku idadi ya watu wasio na kazi nchini humo, ikikadiriwa kuwa zaidi ya asilimia Ishirini na nne, raia wengi wa taifa hilo wamewashutumu raia wa kigeni kwa kuchukua nafasi zao za kazi.

Maelfu ya raia hao wa kigeni, wamekimbia makwao na sasa wanaishi katika kambi za muda, ili hali mataifa jirani wameanza shughuli ya kuwahamisha raia wao.

Siku ya Jumapili, serikali ya Zimbabwe imetuma mabasi kadhaa mjini Durban kwenda kuwachukua raia wake wapatao mia nne.

Takwimu rasmi za serikali zinakadiria kuwa kuna raia milioni mbili wa kigeni wanaoishi nchini Afrika Kusini, lakini wengi wanahoji kuwa idadi hiyo huenda ni kubwa zaidi.

Chanzo: bbc swahili

Monday, April 13, 2015

Zitto: Viongozi wa vyama wasiwe viongozi wa serikali. > Wananchi wamwita msaliti

Kiongozi Mkuu wa ACT Wazalendo Zitto Kambwe akiwahutubia wakazi wa Manispaa ya Iringa
KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe amesema Chamani cha Mapinduzi kinashindwa kutofautisha uongozi wa chama na uongozi wa serikali na kusababisha kuwafanya wananchi kushindwa kujua utendaji wa viongozi hao.

Zitto ameyasema hayo alipokuwa akiwahutubia wakazi wa Manispaa ya Iringa katika Mkutano wa chama hicho uliofanyika katika viwanja vya Mwembetogwa.

Amesema si rahisi kujua utendaji wa kazi za chama na kazi sa serikali kwa Rais Jakaya Kikwete kutokana na kuwa na kofia mbili za uenyekiti wa chama taifa na kofia ya urai wan chi na kwamba haijulikani ni wakati gani anafanya kazi za chama na ni wakati gani anafanya kazi cha taifa.

Amesema nchi inakosa mwelekeo kutokana na kuwapo kwa mfumo wa uongozi wa kinyonyaji na dhuruma unaotokana na viongozi wasiokuwa na maadili ambao kazi yao ni kufanya unyonyaji badala ya kufanya kazi za taifa.

“Ifike mahali ikaeleweka na kutofautisha viongozi wa chama na viongozi wa serikali ili utendaji uweze kueleweka. Si rahisi kutambua Rais Kikwete ni wakati gani anafanya kazi za chama na ni wakati gani anafanya kazi za taifa.

“Mfumo wa uongozi wa namna hii ni wa kinyonyaji kwa kuwa viongozi wengi wanafanya kazi za kinyonyaji kwa kuwa hakuna wa kumkemea mwenzake. Ndiyo maana hata mafisadi wanatazamwa usoni tu kwa sababu mfumo wa uongozi ndivyo ulivyo” amesema.

Amesema mtu yeyote akisema yeye ni kiongozi lazima awe mpambanaji kupigania haki za watu wake kwa ajili ya kuhakikisha watu wake wanakuwa na maendeleo.

Amesema umasikini wa watanzania unasababishwa na wabunge wasiopamba kupigania haki za watu wao na kugeuka kuwa wanyonyaji wasio na huruma.

Amewataka watanzania kuwa kuelewa kuwa si kwamba ufisadi unakwisha bali unaendelea kwa kasi zaidi kwa kuwa serikali iliyopo madarakani imekosa meno kuwashughulikia wezi sugu wanaoiba mali ya umma na kwamba umasikini ni chaguo la viongozi wa kisiasa.

“Umasikini wa Tanzania ni chaguo la viongozi wa kisiasa. Tusipofanya mabadiliko sisi wananchi, umasikini huu utaendelea kuwapo na hautakoma kwa kuwa wenzetu wa chama tawala ndio chaguo lao” amesema.

Amesema tatizo kubwa uchumi umeshikiliwa na watu wachahe ambao hao hao ni viongozia wa kisiasa na wengine ni viongozi wa serikali na kwamba uchumi wa Iringa pia umeshikiliwa na watu wa namna hiyo.